Wachuja Nafaka

Ya Leo Kali

by Wachuja Nafaka

[Chorus]
Ya leo kali...
Ya leo kali....
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
[Verse 1: Dollo]
Stimu ya Kuberi ndo ishaleta matata
We teta' ukiteta
Hujui sisi watu wa nge'ta eeh
Mchana tunalala, lakini usiku tunakesha
Unaweza njoo turuke na masela
Huwezi' wewe sio msela
Wewe umekuwa nani mpaka unasimama kidete
Unatusema sisi ukichoka utawasema viwete
Hii kwa ajili ya kuendekeza njaa kali
Na fainali utakuwa umezusha zali
Ya leo kali' kunguru kanyea ugali' masela wana njaa kali
Wanatoa macho utafikiri wamepoteza nauli
(?) utakuwa mweusi
Kumbe huwajuhi eeh
Una еlimisha wenzako, je umeona mambo yako?
Wajifanya unasoma...unasoma...unasoma...
Chеke'chea, primary , seco' hujawahi kupata vema


[Chorus]
Ya leo kali...
Ya leo kali....
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari we
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
[Verse 2: K.R. Mullah]
Kwa jinsi ulivyoamka tu
Tumegundua ya leo kali
Kwani niliota sana ndoto za hatari hatari
Njaa nliyokuwa nayo ilinitosha kuwaza
Nilikumbuka hadi misosi nliyowahi kuisaza
Ubao unazidi kunicharaza
Kuwasimulia ma braza men; siwezi' najua watakupakaza
Hadi nashika kipaza huko nyuma hali ilikuwa mbaya sana (Mama...! mama...!)
Afadhali hata ya jana kuliko ya leo
Huo msosi wenyewe tu nimeuona kwenye video
Leo ni leo asemaye kesho' mwongo
Maisha haya vijana lazima tuwe na usongo
Hasira' kwani kila unapo amka, mambo bado ni bila bila
Maisha nnayoishi hayalipi
Kutwa nzima leo, nimeshindia pipi
Haya sasa' kuiba naogopa,kuomba naogopa
Wash'kaji wenye nazo wote wamenitosa
Wananiambia niishi ki ghetto ghetto
Eti nisubiri kipindi cha pili pengine ntasaidiwa na upepo
Mi nahaingaika bila mafanikio
Wengi wao nawaeleza matatizo yangu wanaitikia tu, "ndiyo"..."ndiyo"..."ndiyo"
Walala hoi tushukuru sana matumbo hayana kioo
La si hivyo' ingekuwa soo
Kwani tungeona; mipande ya mihogo,maharage hayajaungwa, dona, yaani tungeona kila kona
Wengine siku hizi naskia
Wanatembea na ugali wanasubiri wasafirishe samaki
Najua nkikwambia hii' utakuwa hutaki,ya leo kali
Hivi hawa watu wanaojinyonga hawaoni utamu wa ugali?
We muuza bure' sista duu' kiuno gogo
Inasikitisha sana kila unayepishana nae kapiga mkorogo


[Chorus]
Ya leo Kali...
Ya leo Kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari we...
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
[Verse 3: Juma Nature]
Ya leo kali
Mentali usijali
Kifu kadokoa ugali
Konda kamwambia akachimbe dawa' yeye kaenda kuchimba matofali
Anakwenda pale Mohammedi Hussein anapiga pa-pa-paa-goooal!!!(Crowd Cheering)
Maskini ya mungu kumbe mpira upo katikati
Hacha kunesa nesa, ne-nesa, kwe-kwepa
Ni Chief Kajala reaper, vizingiti tuna vikwepa' kamua
Ni [?] na Sir Nature
Projekta' hafagiliwi mtu' kamulia na nyanya, biringanya,sasa majeruhi ndimu' tamu...
Najaa tokea kanda hii ya ajabu imevuja
Kwa mwenendo wa kilingara
Ni Chief, Sir Nature, Kajala huwapi hasara
Maana mtu tatu timu sisi hatuhitaji reserve
Makeke yake ya hekta hayafikii mwenye gundu
Ma vikatuni ya mbao, na yale yakukatana mundu
Gongeshea kachaa tupate kusogeza siku
Kitakachobakia kingine nafikiri tubakize usiku
Na sijui ka kitabaki' kesho kuna mtu kama laki
Chambua ini, figo, kiwili-wili, utumbo wa ny'a' ubishoo hakuna!
Jinsi kunahela' utu dondoshe wako masela
Hatuna kitu masela tupo empty ile chakara zigi' kibandigi
Pekua kwenye kabati,droo mpaka uvunguni' uzunguni
Haya sasa masela ya leo kali
Kumekucha!
Tutaunguza mwili' lakini zitabakia kucha
Tuandamane masela wangu' kwa staili hii
Tembea kwa mwendo wa pesa' nchi ishauzwa hii


[Chorus]
Ya leo kali...
Ya leo kali....
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali...
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari we
Ya leo kali' mjomba mentali, njoo tutafakari' tupige mistari

Song Comments
On Ya Leo Kali by Wachuja Nafaka

Must have JavaScript enabled to comment.